TEHAMA

TEHAMA ni moja ya vitengo muhimu sana katika utekelezaji wa majukumu ya kikazi hususani kwa kipindi hiki ambacho ni cha mapinduzi ya nne ya kidigitali (4th Digital Industry Revolution). Kulingana na mapinduzi hayo yatupasa kufanya shughuli za chama kwa kujiunga kwenye mifumo mbali mbali ya usimamizi na uendeshaji wa shughuli kama vile mfumo wa MUVU, Mifumo ya manunuzi na usimamizi wa Fedha. Kulingana na mapinduzi haya ya uendeshaji wa ushirika kidigitali imetupasa kuwa na kitengo cha TEHAMA ambacho kinashirikiana na kampuni ya VERIDOC GLOBAL – TANZANIA yenye dhamana ya kufanya kazi za TEHAMA kwenye vyama vya ushirika. Kitengo cha TEHAMA kinamajukumu kama yafuatayo.

  • Kusimamia mifumo ya TEHAMA
  • Kuweka taarifa mpya kwenye tovuti
  • Kurekebisha vifaa vya TEHAMA pale vinapoleta shida(Technical support)
  • Kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu mifumo ya computer
  • Kuingiza wanachama wapya kwenye mifumo
  • Kutoa msaada wa kitalamu pale inapohitajika